Google PlusRSS FeedEmail

MWAKIFAMBA: KIKWETE ANAWAJALI WASANII




Imeelezwa kuwa Rais wa awamu ya nne Jakaya Kikwete amekuwa mstari wa mbele kujitoa kwa wasanii katika matatizo yao hali hiyo inayochangia wasanii wa filamu kuona kuwa rais anawajali na kuthamini mchango wao katika taifa

Hali hiyo imejionyesha pindi wasanii wa filamu wanapopata na matatizo ya kuugua hata msiba, rais anapokuwa karibu nao bega kwa bega

Hayo yalielezwa na Rais wa Shilikisho la Filamu Tanzania (TAFF) Simon Mwakifamba kwa kuonyesha kukubali kazi na ushirikiano wanaoupata kutoka kwa rais Kikwete

Alisema kuwa Rais wa awamu ya nne amekuwa mstari wa mbele kuwasaidia wasanii hali hiyo imetuonyesha kuwa rais anatujali pamoja na kuthamini kazi yetu

"Huyu ni rais wa kwanza kujali wasanii kwa kiasi kikubwa sana, amekuwa mstari wa mbele kuwasaidia, hata kwenye ugonjwa wa Sajuki yeye ndiye aliyekuwa amsafirishe India kwa ajili ya matibabu, hivyo tunajivunia rais huyu kwa kitendo chake cha kuwajali wasanii" alisema Mwakifamba

Mbali na hayo pia amekuwa ni rais wa kwanza kuongoza maelfu ya watu kumzika msanii Sajuki, hali ambayo imeonyesha faraja kubwa kwenye familia ya wasanii wa filamu nchini

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging