Google PlusRSS FeedEmail

MWANAMUZIKI WA BONGO ANAYEFANYA KWELI NCHINI SWEDEN




Mwanamuziki wa kizazi kipya nchini Tanzania Janbert Kiwia 'JanB'anayefanya muziki wake nchini Sweden amekamilisha ujio wake wa albamu yake ya kwanza inayokwenda kwa jina la 360 kwa mwaka

Akizungumza jijini Dar es Salaan JanB alisema kuwa teyari ameshaachia video za nyimbo mbili Pretty Girl na Play haters ambazo zote zinachezwa channel O na katika vyombo vya habari nyingine Afrika Mashariki

Alisema kuwa anafanya muziki wa kileo na anaangalia nini kinatakiwa katika soko la muziki na ndio maana video zake zinafanya vizuri katika ngazi za muziki za kimataifa

Akizungumzia kwa nini video zake zinachezwa channel O tofauti na baadhi ya wasanii walio wengi Tanzania alisema kuwa, kuchezwa kwa video zake channel o ni kutokana na ubora uliopo kwenye video zake

"Video zangu zina ubora wa kimataifa na ndio maana imekuwa ni lahisi kuchezwa channel O ingawa napata shida sana kwa hapa nyumbani bado watu hawajaelewa kazi zangu" alisema JanB

Aliongezea kuwa anajipanga ili aweze kuendelea kufanya vizuri zaidi kwenye gemu la muziki ingawa anaomba ushilikiano kutoka kwa watanzania ili aweze kufanikisha malengo yake



This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging