Wakati Domo Kaya ameachia ngoma yake inakwenda kwa jina la mamiss ngoma ambayoinazungumzia walimbwende ambao huwa wanaiwakilisha Tanzania katika mashindano ya Dunia,
Ipo stori inayovuma kwamba Mandojo ambaye kwa pamoja na domo kaya waliwahi kufanya vizuri katika mziki huu wa kizazi kipya hasa kupitia wimbo wao ‘Nikupe" Joseph Michael ‘Mandojo’ yupo jela huko kanda ya kati Singida
Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali vinasema kwamba msanii huyo amefungwa miaka miwili jela lakini haijabainika ni kisa gani ambacho kimemfanya kupelekwa jela.
Mshirika wa Mandojo, Precioust Juma ‘Domokaya’ wiki iliyopita alibainisha ya kuwa hata yeye amesikia uvumi huo ila bado hajaipata fresh, anachojua ni kwamba mchizi yuko nyumbani kwao Manyoni, Singida kwa ajili ya matatizo ya kifamilia likiwemo lile la kufiwa na baba yake mzazi. “Mi pia sijui chochote kuhusu hilo kwa sababu sijapata simu au taarifa yoyote kutoka huko, siwezi kulizungumzia hilo sana,” alisema Domo.
Tangu wiki iliyopita habari zimekuwa zikizagaa jijini kuwa mchizi huyo ametupwa lupango kwa miaka 2.
Hata hivyo wasanii mbalimbali wakubwa pia wanazungumzia kwamba Mandojo ameingia kifungoni kwa kosa la kupigana hadharani na watu wasiojulikana
Pro-24 inaendelea kufuatilia kwa makini habari za bingwa huyu na itakuwa ikiku-update kila inapopokea habari mpya..
PRO24 RADIO/TV
CLICK AND ENJOY GOOD MUSIC
MIXTAPES
ARTIST PROFILES
Blog Archive
LOVE LINKS
PRO-24 DJS OFFICIAL BLOG
PRO24 ENTERPRISES. Powered by Blogger.








