Google PlusRSS FeedEmail

Q CHILLAH AUNGANA NA VISUAL LAB

Msanii mwenye vipaji vingi katika game hili la Bongo Fleva Q. Chillah ameiambia pro-24 web kuwa kwa sasa kazi zake za visual zote zinasimamiwa na Adam Juma wa visual lab  Mbali na Adam Q.Chief amesema bado anaendelea na mkataba wake na Didaz Fashion jamaa ambaye anaishi huko kwa malkia  UK ambaye yeye ndiye anamtafutia Q Chillah show za nje ya Tanzania.

Q Chillah aliongeza kwa kusema Adam wa visual lab  hakukosea kunichagua maana kwa miaka mingi nilikuwa natamani sana kuwa hapo
Kwa sasa watu wawe wananisikilizia na kuniona kwenye video zitakazokuwa na ubora wa hali ya juu na mpaka sasa  tumeshafanya video kadhaa zitaachiwa soon"
Mbali na hiyo Chillah aliongeza kwa kusema  tarehe 29 mwezi huu atakuwa na show mkoani  Tanga, kwenye ukumbi wa Tanga Beach Resort, na show hiyo itakuwa Live Band na ataongozana na wasanii wengine wanaofanya  Bongo fleva, akiwemo Rais wa Ma Sharobaro Bob Junior. Hii itakuwa show ya kuhamasisha vijana kupiga kura siku ya tarehe 31 mwezi huu..

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging