Fred Maliki ‘Mkoloni’ mmoja wa wasanii wa kundi hilo, anachana live bila chenga kuwa, kundi hilo limeamua kuendeleza harakati zao, hivyo hawatachoka kupiga kelele kulalamikia ufisadi au kupinga huduma mbovu, hadi wahusika watakapojirekebisha.
Alisema, ni kutokana na uamuzi huo, ndio maana wameamua kutoa sehemu ya pili ya wimbo wao huo, lengo likiwa kuwakosoa viongozi na watendaji wasiotimiza wajibu na dhamana walizopewa.
“ baada ya kufanikiwa kukamilisha kampeni zetu kwa ndugu yetu Sugu, sasa tunarejea katika kampeni zetu dhidi ya mafisadi, hatutachoka , tumeachia albamu mpya ya Anti Virus Vol 2,” alisema Mkoloni.
Alisema, wamepania kuisambaza kila pembe ya nchi, ili kila Mtanzania popote alipo aweze kuipata kazi hiyo ambayo imebeba ujumbe mzito.








