Google PlusRSS FeedEmail

MARA BAADA YA BODI YA FILAMU KUANZA KAZI MAMBO YAKO HIVI

                

Baada ya Bodi kuingia kuanza kazi  rasmi baadhi ya watayarishaji wameanza kuonja sumu za Bodi hiyo kwa kukiuka sheria na taratibu za utengenezaji wa filamu kwa mujibu wa sheria ya filamu ya mwaka 1976 nambari 4, mmoja wa mwadhirika wa awali ni kampuni ya Al – Riyamy Production ya Jijini Dar es Salaam baada ya zaidi ya filamu zao 5 kukutana na msemeno huu.
Filamu zilizokaguliwa na kukutwa na ukiukwaji wa maadili ni pamoja na filamu ya Mtoto wa Mamafilamu ambayo ilielekeza kuhamasisha tabia za ushoga kwa kuigiza tabia za kishoga, jambo ambalo linapingana na maadili ya Mtanzania kwa mujibu wa sheria za Tanzania.
Filamu nyingini ni Iny’e, Iny’e Plus, Iny’e Gwedegwede filamu hizi ambazo zimeigizwa na wachekeshaji zimeonekana kudhalilisha wakina mama kwa kuonyeshwa sehemu za miili yao na katika ukaguzi filamu hizi zilipewa daraja la R (Rated R) ambalo filamu zake haziruhusiwi kuonyeshwa katika jamii yetu.

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging