Msanii nyota ndani ya bongo movie Vicent Kigosi ‘Ray’ amesema kuwa anatarajia kutoa Filamu yake mpya aliyocheza na binti machachari Elizabeth Michael ‘Lulu’ ambayo itakuwa sokoni baada ya kazi ya ‘Sobbing' kutoka . Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na chombo cha habari hapa jijini Ray alidai kuwa filamu hiyo ipo katika hatu ya mwisho kumalizika hivyo anaamini itafanya vizuri baada ya kwenda sokoni.Ray alisema filamu hiyo ilitengenezwa kabla ya Lulu kupata matatizo hivyo ilikuwa katika sehemu ya mwisho ya kuihariri , Pamoja na hayo msanii huyo alidai kuwa haitaji kutoa kazi kwa kukurupuka kwani mipango yake ni kulifanya soko la filamu nchini liweze kufika mbali“Sihitaji kutoa bora filamu kwa sababu katika tasinia hii watanzania wanahitaji kuona kazi zangu zenye ujumbe ambao unawez kudumu miaka mingi” alidai
PRO24 RADIO/TV
CLICK AND ENJOY GOOD MUSIC
MIXTAPES
ARTIST PROFILES
Blog Archive
LOVE LINKS
PRO-24 DJS OFFICIAL BLOG
PRO24 ENTERPRISES. Powered by Blogger.







