Google PlusRSS FeedEmail

UPELELEZI HAUJAKAMILIKA KESI YA LULU





Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam imeambiwa na upande wa Jamhuri kuwa upelelezi wa kesi dhidi ya msanii wa filamu Elizabeth Michael (18) maarufu ‘Lulu’anayekabiliwa na mauaji ya msanii mwenzake Steven Kanumba (28) bado haujakamilika

Kesi hiyo ilitajwa jana mbele ya Hakimu Augustina Mmbando ambapo upande wa Jamhuri unaendelea kuieleza mahakama hatu za upelelezi wa kesi hiyo, kwamba bado unaendelea

Hakimu Mmbando alisema kesi hiyo itatajwa Oktoba 8 mwaka huu na mshtakiwa ataendelea kukaa mahabusu

Aidha kwa mujibu wa Mwenendo wa Sheria ya Makosa ya Jinai (CPA), Lulu hakutakiwa kujibu chochote kwa kuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi za mauaji lakini mara upelelezi wake utakapokamilika itahamishiwa Mahakama Kuu Tanzania , Kanda ya Dar es Salaam

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging