PASTOR MYAMBA KUYAANIKA MAISHA YA WALOKOLE KWENYE FILAMU
Wasanii wa filamu wameamua kuanika maisha ya walokole kwa kuandaa filamu itakayoonyesha maisha ya baadhi yao wanavyoishi kinyume na maadili ya mungu
Filamu hiyo iliyoitwa 'Chegue in The Bible'itakayomshirikisha msanii Pastor Myamba na msanii nyota Ndumbangwe Misayo 'Tea'
Akizungumzia juu ya filamu hiyo Myamba alisema "kuna mambo mazito tutayaonyesha kama vile misukosuko ya maisha ya wanandoa, kuna mjane na mwanaye ambaye ameendekeza anasa" alisema Myamba








