TUZO za Mama Shujaa wa Chakula 2021-2013, zimekamilika juzi usiku baada ya Sister Martha Mwasu kutoka Kondoa kuibuka mshindi wa kwanza na kujinyakulia zawadi ya vifaa vya kilimo vyenye thamani ya shilingi milioni 10
Sister Mwasu aliibuka kidedea kwa kuwaangusha washiriki wenzie 13 walioingia katika kinyanganyiro hicho kutokana na kuwa na juhudi na ubunifu mkubwa aliouonyesha kwa kipindi cha wiki mbili alizokuwa akiishi katika kijiji cha Maisha Plus zilizomsababisha kupata kura nyingi kutoka kwa wananchi
Nafasi ya pili ilishikiliwa na Bi.Emilian Eligaisha kutoka Karagwe na kupewa zawadi ya vifaa vya ujenzi vya milioni 3, nafasi ya tatu ikichukuliwa na Bi. Tatu Abdi Kutoka Lushoto ambapo alipewa shilingi 700000
Akizungumza wakati akikabidhi zawadi kwa mshindi wa tuzo ya hiyo Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Bw. January Makamba alisema kuwa kuna kila sababu ya kuboresha mazingira rafiki kwa wakulima hususani kwa akina mama kwani shunguli zote za kilimo zinafanywa na wanawake
Alisema kuwa Fikra dume, sera dume, pamoja na mipango dume huzaa matokeo dume hii inasababishwa na kuleta utofauti wa jinsia katika utekelezaji na uwajibikaji wa maendeleo
Makamba alisema kuwa asilimia 95 ya chakula tunachokula kinazalishwa na akina mama, cha kushangaza asilimia 99 ya wasiyozalisha chakula ndio wanaomiliki ardhi, na kusababisha kuwa na unyanyasaji wa kijinsi unaomgusa moja kwa moja mwanamke







