Google PlusRSS FeedEmail

WOLPER KUTOKA NA FILAMU YA KUMUENZI KANUMBA



DIVA wa filamu za kibongo Jacqueline Wolper anatarajia hivi karibuni kutoka na movi inayokwenda kwa jina la 'After Death'kwa ajili ya kumuenzi marehemu Steven Charles Kanumba

Akizungumza na jarida la Maisha jana jijini Dar es Salaam, Wolper alisema kuwa ameamua kutoka na filamu hiyo kwa sababu ya kumuenzi kwa vitendo msanii mwenzie marehemu Kanumba

Alisema filamu hiyo inaelezea maisha ya marehemu Kanumba baada ya kifo chake, ndani ya filamu hiyo ameigiza na watoto wawili ambao walikuwa wakiigiza na marehemu Kanumba

"Kwenye filamu hiyo nimeamua kuigiza na wasanii wengi ambao walishawahi kufanya kazi na marehemu kanumba, na nimeamua kufanya hivyo kwa sababu ya kumuenzi marehemu kwa vitendo na ukiangalia nimefanya naye kazi nyingi ikiwemo ile ya mwisho 'Ndoa yangu' hivyo nina kila sababu ya kufanya hivyo" alisema Wolper

Mbali na hayo alisema kuwa ameamua kujitolea kuwaendeleza Patrick na Jenifer ni watoto ambao walikuwa wakifanya kazi na marehemu Kanumba ili kuendeleza vipaji vyao kwani hakuna mtu aliyejitokeza kufanya hivyo

Alisema kuwa ni vizuri kuviendeleza vipaji vya watoto hao kwani mwenye marehemu alikuwa na ndoto ya kuinua vipaji chipukizi ili kuikuza tasnia ya filamu nchini Tanzania

"Kwa kuwaendeleza watoto hao kwangu mimi ni faraja kubwa kwani naamini sasa namuenzi kwa vitendo kwa sababu kitu ninachokifanya ndicho yeye alikuwa akipenda kukifanya kila wakati na alikuwa na ndoto ya kukuza vipaji vya chipukizi' alisema Wolper


This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging