Justin Bieber (18) na Selena Gomez (20)wanaonekana kuzima
kabisa tofauti zao na sasa wanaonekana kula ‘bata’ huku picha mpya zilizopigwa
wiki hii zimeainisha kurejea kwa mahusiano yao
Wapendanao hao wameamua kutoa nafasi nyingine kwa penzi lao
ambalo lilikaribia kuvunjika hivi karibuni baada ya kimwana huyo kumtuhumu
Bieber kumchombeza vimwana wengine kwa kutumia simu yake
Wakati wakiwa katika ziara ya mapumziko Selena alipigwa
picha akiwa amekaa mapajani mwa Bieber huku wakibusiana na kukumbatiana wakati
wakisubili usafiri kwenye Uwanja wa ndege wa Salt Lake City Utah