FM ACADEMIA KUFANYA KWELI MSASANI BEACH
Rais wa bendi ya muziki wa dasni ya FM Academia 'wazee wa ngwasuma' Nyoshi el Sadaat amesema wamejiandaa kikamilifu kuvurumusha burudani ya nguvu katika sherehe ya kuadhimisha miaka 15 zitakazofanyika katika Ukumbi New Msasani Beach Club
Akizungumza na waandishi wa habari Nyoshi alisema wamefanya mazoezi ya kutosha kuhakikisha wanawapa raha mashabiki wa bendi hiyo ambao wanawaunga mkono kwa muda mrefu licha ya kupita milima na mabonde hadi kufika hapo walipo
Alisema kuwa wamewatayarishia mashabiki nyimbo mpya ikiwa kama zawadi kwao katika kipindi hiki cha kumalizia mwaka
Nyoshi alisema katika sherehe hiyo watapiga nyimbo za zamani zilizopo katika albamu yao ya kwanza hadi ya mwisho ambayo ni vuta ni kuvute








.jpg)