Google PlusRSS FeedEmail

ROSE NDAUKA AFAFANUA UREMBO WAKE



Naye msanii wa filamu Rose Ndauka pia ameweka wazi kuwa kunywa maji kwa wingi pamoja na kupumzika ndiyo siri ya urembo wake

Alisema pia hata kufanya mapenzi  anaratiba ili asiharibu mwili wake huo hivyo anazingatia sana hilo na ndio siri ya mafanikio yake

Msanii wa muziki wa bongo fleva Barnaba yeye alisema kinachomsababisha kuendelea kuonekana na afya njema na muonekano nadhifu ni kutotumia kilevi cha aina yoyote na kufanya juhudi katika mazoezi yake

"Mimi najitahidi sana kufanya mazoezi na kula vizuri  huku nikiwa na ratiba maalumu ya  kukutana na mpenzi wangu kimwili na sijawahi kutumia kilevi chochote kile " alisema Barnaba

Naye msanii wa filamu na bongofleva Shilole alisema anaonekana bado na mvuto kwa sababu ametenga masaa matatu ya kupumzika kila siku na hupendelea kula ugali samaki na mboga za majani

Alisema mbali na hilo pia anakuwa makini na chaguo la mafuta anayoyapaka ili aweze kuendelea kubaki na ngozi yake






This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging