GAGA ASOGEZA MBELE ZIARA YAKE YA MUZIKI
Mwanamuziki mwenye vituko kila kukicha Lady Gaga ameendelea kusogeza mbele ziara za kutangaza muziki wake wa 'Born This Way Ball tour'
Rafiki wa karibu wa msanii huyo amesema kuwa amesogeza mbele ziara hiyo hadi septemba mwaka huu kutokana na hali yake kuwa bado sio nzuri
"Yupo Chicago ndani ya uangalizi wa mpenzi wake Taylor Kinney, ingawa kwa sasa anaendelea vizuri na anaweza kutembea taratibu teyari daktari wake amesema bado anahitaji kupona zaidi" alisema
Gaga amelazimika kuhairisha ziara hiyo mara mbili kutokana na kuumia nyonga na kufanyiwa upasuaji ambapo hali yake inaendelea vizuri licha ya kuwa bado yupo kwenye uangalizi wa madaktari








