Google PlusRSS FeedEmail

KIINGEREZA KITATUFIKISHA KWENYE KILELE CHA MAFANIKIO KAMA YA WENZETU

                                     Hashim-Kambi

Mahiri wa filamu Bongo Hashim Kambi ‘Ramsey’ amedai kuwa waigizaji wa filamu wanahitaji kujifunza lugha hasa kiingereza ili kufikia katika soko la kimataifa, Kambi anaamini kuwa endapo wasanii wa filamu watajua Lugha zaidi ya Kiswahili uwezekano wa kufanya vizuri na kufikia katika medani za kimataifa.

.“Nimetembea na kujifunza mengi wasanii wa Tanzania wengi tuna vipaji vya hali ya juu katika uigizaji lakini inawezekana tatizo letu lipo katika soko letu kwa kazi zetu, nimeongea na mwigizaji wa kimataifa kutoka nchini Ghana Van Vicker amenishauri umuhimu wa wasanii wetu kujua Kiingereza ikiwezekana kurekodi hata filamu itakayotumia lugha hiyo,”anasema Ramsey.

Hivi karibuni msanii Ramsey alimleta msanii kutoka nchini Ghana Van Vicker na kurekodi naye filamu yake akishirikiana naye lengo likiwa kulikata soko la kimataifa au kujenga ushirikiano na msanii huyo kwani awali Mzee Kambi aliwahi kwenda nchini Ghana kushiriki filamu ya Van Vicker akiigiza kama daktari katika filamu hiyo.

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging