WEMA NA DIAMOND HII NI FILAMU AU KWELI?
IKIWA ni siku chache baada ya msanii wa muziki wa kizazi kipya nchini Nassib Abdul 'Diamond Platnum' kukanusha vikali juu ya kurudiana na aliyekuwa mpenzi wake wa zamani Wema Sepetu na kumbwaga mpenzi wake wa sasa mtangazaji wa DTV Dvj Penny picha za wawili hao zaonekana wakiwa katika pozi la kimahaba.
Diamond alituma picha inayomuonesha akiwa katika pozi la kimahaba na msanii huyo Wema Sepetu kupitia ukurasa wake wa Instagram na kudai kuwa wawili hao wapo 'Location' kwa ajili ya kutengeneza movi aliyoandika kwa jina la 'Temptations'.
Diamond alituma picha hiyo na kuandika kuwa "katika moja ya movi ambazo naimani itakuwa ni gumzo, na mfano bora toka Tanzania hii Temptations' Star Tune soon" hayo ni maneno aliyoandika msanii huyo kupitia ukurasa wake wa Istagram.








