KIFO cha rais wa Afrika Kusini Nelson Mandela kimewagusa mataifa yote duniani, watu kutoka mabara yote huku kila mmoja akionesha kuguswa kwake kwa njia tofauti tofauti.
Katika kuonesha masikitiko na majonzi ya msiba huyo rapper The Game ameamua kuchora tattoo ya sura ya Mandera itakayokaa kwenye mwili wake kwa muda mrefu.
Rapper huyo ameamua kuchora tattoo hiyo kwenye mgongo wake ikiwa kwa nia ya kumuenzi ambapo baada ya kuchora amezituma picha hizo kwenye ukurasa wake wa Instagram.