MUIMBAJI wa muziki wa kizazi kipya nchini Elisha Simon 'Hisia' hivi karibuni anatarajia kuachia nyimbo yake mpya itakayojulikana kwa jina la 'Mawazo' , ambayo imebeba ukweli wa jambo lililowahi kumtokea katika maisha yake.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi akiwa nchini Nairobi, Hisia aliweka wazi kuwa hivi sasa yupo katika maandalizi ya mwisho ya kutengeneza nyimbo hiyo ambayo ameitengeneza katika mtindo tofauti na uliozoeleka.
Nyimbo hiyo ambayo itakamilisha nyimbo mbili tangu amalize mashindano ya Tusker Project Fame, Hisia aliweka wazi kuwa nyimbo hiyo imetengenezwa tofauti na anaamini itafanya vizuri.
Alisema kuwa nyimbo hiyo imefanywa 'live' ambapo vyombo vyote vya muziki vitasikika hali hiyo itasababisha nyimbo hiyo kuonekana yenye utofauti na mvuto wa kipekee.
Akielezea alichokiimba kwenye nyimbo hiyo Hisia alidai kuwa nyimbo hiyo ni ya historia ya kweli ambayo teyari ilishawahi kumtokea kwenye maisha yake, ingawa imemtokea mara baada ya kumaliza kuiandika nyimbo hiyo.








