Wanamuziki wawili wa kike kutoka nchini Marekani Rihanna na Shakira wapo katika maandalizi ya kuachia nyimbo yao kushirikiana iliyopewa jina la 'Can't Remember to Forget You', January 13 mwaka huu.
Maandalizi hayo ambayo yanaonekana yapo katika hatua ya mwisho ambapo Shakira ameonesha muonekano wa kava la wimbo huo utakavyokuwa ambapo alituma ujumbe kwenye ukurasa wake wa Twitter na kuandika 'Yuo guys ready? jan 13 is almost here,".
Wimbo huo utakuwa wa kwanza kutoka kwenye albamu mpya ya Shakira, ambapo msanii huyo alishawahi kumshirikisha Beyonce kwenye wimbo wa 'Beautiful Liar'.








