Google PlusRSS FeedEmail

HATIMAYE JUSTIN BIEBER ABATIZWA

Justin Bieber ameamua kufuta dhambi zake zote na kuzaliwa mara ya pili kwa kubatizwa na kujiunga rasmi na imani ya kikristo. Ubatizo umefanyika bafuni kwa rafiki yake.

Mwimbaji huyo mwenye umri wa miaka 20 amechukua uamuzi huo iki ni wiki siku chache zimepita tangu zivuje video zinazomuonesha akifanya utani wa kiubaguzi wa rangi alipokuwa na umri wa miaka 15.

Mchungaji Carl Lentz aliyembatiza Justin Bieber ameiambia TMZ kuwa alitumia wiki moja kufanya mafundisho ya kina ya biblia na Justin Bieber mwezi uliopita kabla video za kibaguzi hazijavuja, na ilikuwa ni siku chache kabla hajafuatwa na mtu aliyetaka ampe dola milioni moja ili asizitoe video hizo.

Ameeleza kuwa Justin Bieber amekuwa akisoma Biblia mara kwa mara na kuhudhuria mafundisho ya dini lakini alikuwa hajapata kanisa ambalo angeweza kubatizwa bila kuingiliwa hivyo aliamua kuchagua kufanya ubatizo huo ndani ya bafu la rafiki yake(ndani ya bathtub) ili kuweka usiri.

Katika hatua nyingine, Usher Raymond amemtetea Justin Bieber kuhusu video za kibaguzi zilizovuja na kudai kuwa Justin sio mbaguzi wa rangi hata kidogo na kwamba alikuwa mtoto mdogo asiye na ufahamu wa madhara ya utani wake.

Usher ameandika kwenye Instagram:

“At my core, I am a person that supports growth and understands without judgement, that growth often comes as a result of pain and continues effort. As I have watched Justin Bieber navigate difficult waters as a young man, I can tell you that he hasn't always chosen the path of his greatest potential, but he is unequivocally not a racist. What he was 5 years ago was a naive child who did not understand the negative power and degradation that comes from playing with racial slurs. What he is now is a young man faced with an opportunity to become his best self, an example to the millions of kids that follow him to not make the same mistakes.”

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging