Google PlusRSS FeedEmail

RIHANNA APEWA TUZO

Wiki moja baada ya kushinda tuzo ya mitindo ya CFDA kama ‘Fashion Icon of the Year’, Rihanna ametajwa pia katika tuzo za Guys Choice Awards kama ‘Most Desirable Woman’.

Tofauti na ilivyokuwa kwenye CFDA alipozua balaa kwa vazi lake, Rihanna alipanda jukwaani kupokea tuzo hiyo akiwa amevaa vazi la heshima.

Rihanna alikabithiwa tuzo na mchekeshaji wa Marekani Kavin Hart ambaye alipomuona aliweka utani kama kawaida yake, “Ni wanaume wangapi wamekasirika kuwa hayuko mtupu?”

“Sawa, namaanisha, asanteni kwa kunipigia kura kushinda tuzo hii nikiwa na umri wa miaka 26 kwa sababu wote tunafahamu inaenda chini zaidi kutoka hapa. Lakini hii ni tuzo ya ucheshi, niappreciate.” Alisema Rihanna.

“Shout Out to all real men out there.” Rihanna alisema kwa kumalimalizia.

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging