Shabiki maarufu wa Michael Jackson ambaye alikuwa ni Mfalme
wa Musiki wa Pop ambaye kwa sasa ni marehemu, ametumia zaidi ya pauni za
Uingereza 2000 (sawana shilingi za Tanzania 5,590,621) kuchubua ngozi yake ili
kufanana na mwanamuziki huyo.
Shabiki huyo Mbrazil, Antonia Gleidson Rodrigues, 32 ambaye
amejitangaza kuwa mtu pekee anayefanana na Michael Jackson kuliko wote nchini
Brazil, amefanyiwa upasuaji ili kufanana na Michael huku akitumia zaidi ya saa
4 kila siku kujifunza kucheza filamu na muziki kama Michael Jackson.
“Gleidson Jackson”, kama ambavyo hupenda kuitwa, alifanyiwa
upasuaji mara ya kwanza miaka mitano iliyopita, ambapo alirekebishwa pua ili
aweze kuimba sauti ya juu.
Baada ya upasuaji wa kwanza, mkazi
huyo wa Fortalenza, Brazil aliendelea na mkakati wake wa kufanana na mwanamuziki
huyo wa pop kwa kudungwa tindikali ili kuufanya uso wake kuwa mweupe, pamoja na
sindano zilizofanya maeneo yanayo zunguka macho kubadilika.
Gliedson ambaye alikuwa mwalimu wa
maigizo, alifanyiwa upasuajia ili kuziba nafasi zilizopo meno yake, kurekebisha
kope kwa kuzichora kama tattoo. Sasa hivi shabiki huyo anakusanya pesa kwa
kumuigiza Michael Jackson ili aweze kulipia upasuaji mwingine zaidi.
Anasema: “Kama nitamudu gharama, nafikiria kufanyia kazi
magego iliniondokane na mikunjo ya mdomoni – nataka pia kuchonga nyusi.
Ningependa pia paji langu la uso lichorwe (tattoo) na kuchonga pua yangu iwe
nyembamba zaidi.”
Gleidson alivutiwa kuwa kama Michael
Jackson alipokuwa na miaka 19 baada ya mwanafunzi mwenzake kumwambia anafanana
na mkongwe WackoJacko. “Ilikuwa ngumu, nilitaniwa kwa siku 15. Mwishowe
nikanasa – nikaambukizwa.”
Gleidson anasema kwa sasa alivyo na
anavyojitahidi kuwa ni zawadi tosha anayoweza kumpa supastar Michael ambaye kwa
sasa ni marehemu. “Katika matamasha yangu huwa nnasema hakuna kopi
inayoweza kuwa nzuri kama origino, Pamoja na hayo nitajitahidi kuwa na kufikia
vilele vya ubora – kama Michael”