“TAFF inadili issue muhimu hatuhangaiki na mbwembwe za kujinuisha na misiba au matamasha, tunaangalia mustakabali wa Sanaa yetu, na tumefanya lobbying kwa waheshimiwa Wabunge kwa mara ya kwanza tasnia ya filamu na muziki itaongelewa katika katiba,”anasema Mwakifwamba.
Rais huyo amedai kuwa shirikisho lao limekuwa mbele kupigania maslahi ya wasanii wote pasipo ubinafsi wa kujitengenezea fedha kwa kutumia wasanii na wanaonufaika ni wachache na kuichafua tasnia nzima na kuonekana haifai ikiongoza kwa kashfa.