Google PlusRSS FeedEmail

KAMANDA ATHIBITISHA CHIDDI BENZ KUKAMATWA NA DAWA ZA KULEVYA UWANJA WA NDEGE





MSANII wa muziki wa kizazi kipya nchini, Chiddi Benz amekamatwa na dawa za kulevya ndani ya Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere akiwa anaelekea jijini Mbeya kwenye show ya Instagram Party ambayo ilikuwa ikitarajiwa kufanyika kesho.

Msanii huyo amekamatwa leo mchana akiwa katika sehemu ya kuondokea ambapo alifanyiwa uchunguzi katika maungo yake na kukamatwa na kete 14 alizokuwa ameweka katika mfuko wa shati lake na misokoto miwili ya bangi na vifaa vingine vinavyohusisha na masuala ya uvutaji dawa za kulevya.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Kamishina Msaidizi wa Polisi ambaye pia ni kamanda wa Viwanda vya ndege Tanzania Hamisi Selemani alieleza kuwa msanii huyo alikiri kuwa dawa hizo ni za kwake na kwamba anatumia dawa hizo.

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging