Nyota wa muziki wa Pop,Nick Minaj ,amefurahiswa na hatua ya Beyonce,Kumtumia ujumbe mfupi wa maneno wakati wa kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa
Msanii huyo machachari aliadhimisha majuzi na kufanya tafrija fupi iliyohudhuriwa na baadhi ya watu maalumu walioalikwa
mwanamuziki huyo alisema kuwa alifurahishwa sana kwa kuwa anaamini Beyonce,anamthamini kwa kiasi kikubwa katika siku yake ya kuzaliwa
Minaj msanii mwenye vituko lukuki ndani na nje ya jukwaa,alisherehekea siku yake kuzaliwa mara baada ya kufikisha umri wa miaka 32.