Mwanamitindo Naomi Campbell amejiunga na wasanii mbalimbali kwa maandalizi ya filamu mpya ya wanamitindo inayotarajiwa kutoka hivi karibuni..
Nyota huyo wa zamani wa urembo ,aliungana na wasanii maarufu mbalimbali akiwemo Kyle Minogue,Foxy Brown , na Tyson Beckford,katika hafla fupi iliyofanyika New York Marekani
Msanii huyo aliyetamba katika miaka ya 1980 na mwanzoni mwa miaka 1990,ameonekana bado ana mvuto mkubwa
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 44 sasa anatarajia kuanza kuonekana filamu mpya inayotengenezwa na mtayarishaji Lee Daniels
Naomi anatajwa kuwa mmoja wa wanamitindo waliotia fora katia tasnia hiyo kutokana na umbo lake la kuvutia