MAPEDESHEE WAMTOLEA UDENDA LULU
Staa wa Filamu za Kibongo Elizabeth Michael ‘Lulu’ hivi karibuni alijikuta kwenye wakati mgumu baada ya mapedeshee wa Bukoba kumganda na kumzonga huku kila mmoja akitaka namba yake ya simu. Lulu aliongozana na wasanii wengine akiwemo Kulwa Kikumba ‘Dude’ kwenye uzinduzi wa hoteli iitwayo Nalfin iliyozinduliwa juzikati wilayani Muleba ambapo staa huyo alionekana kuwaumiza vichwa wanaume wakware wenye fedha zao.