“Waongozaji wa filamu ni wachache au naweza kusema kuwa ni wale wale, kila siku wasanii wanzuri wanaibuka na kuwika lakini ni vigumu hali hiyo kutokea kwa waongozaji wapya na kufanya vinzuri, tunahitaji basi watoke hata nje ya nchi kuepusha upendeleo kwa baadhi ya wasanii,”anasema Lulu.
Lulu anasema hiyo ndio moja ya sababu inayofanya wasanii wengi kutengeneza filamu zao wenyewe kama waongozaji na hata kuwa ndio watayarishaji wakuu baada ya kukosa nafasi mara kwa mara, hivi karibuni Lulu amefanikiwa kutoa filamu yake Mapenzi ya Mungu aliyomshirikisha Mama Kanumba ikiwa ni moja ya kazi zake ambazo amekuwa akiziandaa mwenyewe.