Nyota wawili wa muziki wa Hip Pop Nchini Marekani P.Diddy na Drake hivi majuzi walionekana wakitishiana maisha ,mara baada ya kurushiana maneno makali katika klabu ya Fontainebleau Hotel huko Miami,Marekani
Wasanii hao walianza kurushiana maneno asubuhi walipokuwa wakitoka katika club hiyo ya usiku ambapo inasemekana chanzo ni P.Diddy kutoa maneno ya kashfa kwa Drake alipokuwa Jukwaani
Hata Hivyo mtayarishaji wa muziki Boi-1d,aliomba wasanii hao kufanya wimbo wa pamoja ambapo Drake alionekana kutokubaliana na jambo hilo..
Taarifa kutoka vyazo mbalimbali vya habari zinasema kuwa P.Diddy na Drake wamekuwa katika kutoelewana kutokana na Drake kuhusishwa kuwa na usiano wa kimapenzi na Cassie ambaye ni mpenzi wa P.Diddy