“Nafurahia kuigiza na wasanii wakubwa wanaofanya vizuri kama Jb kitu ambacho kinanifanya nijione kiwango changu kipo juu sana kwani nakutana na wasanii wenye uwezo na kukubalika katika filamu,”anasema Cassie.
Msanii huyo kutoka Zambia amecheza katika kampuni ya Jerusalem Film awali alishiriki katika filamu ya Vita Baridi na mwaka huu ameshiriki katika filamu mpya inayokuja ya Mzee wa Swaga akiwa na msanii mkongwe anayefanya vizuri katika game