Google PlusRSS FeedEmail

KITABU CHA KANUMBA KUZINDULIWA

                         
KITABU cha historia ya maisha ya mwigizaji nyota  Hayati Steven Kanumba kinatarajiwa kuzinduliwa tarehe 10 January 2014 katika ukumbi wa Landmark Ubungo, uzinduzi huo utaambatana na maonyesho ya kazi za marehemu Kanumba alizowahi kushiriki na kuzifanya.


Mama yake mzazi akiongea na FC amewashukru wale wote ambao wamekuwa wakijaribu kufanya kazi ambazo kwa njia moja au nyingine zinamkumbuka mwanaye ambaye aling’ara katika tasnia ya filamu  na kufanikiwa kutangaza Tanzania.
                 
“Nawashukru sana watanzania na wale ambao si Watanzania wamekuwa faraja sana kwangu, hasa pale ambapo wamekuwa wakiona umuhimu wa kumuenzi Kanumba kwa njia tofauti tofauti, nawashukru sana, na najua kila mtu ana mchango mkubwa si rahisi kuwataja majina maana mpo wengi,”anasema mama Kanumba.

Kitabu hiki kinachohusu maisha ya Kanumba The Great Fallen Tree kimeandikwa na E. Emmanuel kutoka nchini Canada na kuhaririwa nchini Marekani na kufanyiwa uchapishaji nchini Kenya
Uzinduzi wa kitabu utasindikizwa na Christian Bella na Bendi ya Malaika kiingilio ni Ths. 20,000/ na utapata kitabu kimoja bure ukiingia tu mlangoni na kazi zote za Hayati Kanumba zitapatikana siku hiyo. USIKOSE TUKIO HILI LA AINA YAKE!

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging