Mtarishaji wa Video Nchini Adam Juma amewataka wasanii kuwalipa vizuri ili wapate Video Bora, akizungumza jijini Dar es salaam jana alisema wasanii wanapenda vitu vizuri lakini hawataki kulipa.aliongeza kwa kusema kuna Video zinategemewa kutoka hivi karibuni ikiwa pamoja na Chege na Mh Temba ambazo zilifanyika Africa ya Kusini.
Akitoa mwito kwa wasanii kuwa na bajeti nzuri na kwamba bajeti itakapokuwa ya kiwango cha chini na video nayo inakuwa ya kiwango cha chini.