“Nilipatwa na hofu nikitaka kuamini kuwa labda swahiba yangu Marehemu Kanumba kaondoka na nyota yangu na hilo lilitokana na ukaribu na marehemu kwani ilikuwa kila akitoa sinema anaichagua na kushiriki, nashukru nimepata meneja na tayari nimerekodi filamu kadhaa,”anasema Kimlola.
Kimlola anasema amesharekodi filamu mbili ambazo tayari amepokelewa na wasanii vizuri na wenzake kwa kiwango cha juu hata kutishia nafasi za wasanii kama Ritchie na Lumole Matovolwa alioshiriki nao katika filamu ya Bahati na filamu ya Ndio Ilivyo.