“Wazo la Mkude Simba nilikuwa nalo toka mwaka 2012 lakini nilipokuwa najaribu kulitumia baadhi ya Redio zilishindwa kunielewa, lakini Efm walinielewa na kutumia vibwagezo vyangu vya Mkude Simba,”anasema Kitale.
Kitale anasema kuwa baada ya kufanikiwa kujenga alama ya uhusika wa mtumiaji wa madawa ya kulevya ‘Teja’ alikuwa akiumiza kichwa anaweza kuibuka na kitu gani cha kibunifu na kuteka hadhira, katika kulinda kazi zake anatarajia kufungua kampuni yake na kazi yake ya kwanza itakuwa Harusi ya Teja.