TID HATIHATI KUSEKWA JELA KWA MARA YA 2.
Staa wa Bongo Fleva anayesumbua na wimbo wa Chumvini, Khaleed Mohamed ‘TID’ amehusishwa na msala mwingine baada ya kudaiwa kumjeruhi James Richard, mkazi wa Jiji la Dar.
Endapo itathibitika kama ni kweli ametenda kosa hilo, TID atakuwa yupo katika hatari ya kuswekwa gerezani kwa mara ya pili kwani mwaka 2008 alitiwa hatiani kwa kosa la kumpiga Ben Mashibe, mkazi wa jijini Dar ambapo alifungwa jela mwaka mwaka mmoja na baadae kutolewa kwa msamaha wa Rais.
SOURCE:GLOBAL PUBLISHERS