Google PlusRSS FeedEmail

ONE ORGANIZATION MARA NYINGINE NA ONE CAMPAIN

                                        

One Organization kwa mara nyingine tena wanaendelea kuelimisha na kuburudisha na kuwaunganisha Africa chini ya project yao "One Campain", baada ya kuwakutanisha wasanii wakike wakubwa Africa na kutengeneza wimbo pamoja na video kupunguza umaskini Africa "Poverty is Sexist".

Safari hii campaign hii inajumuisha wasanii wakike tu ukiringanisha na mwaka jana ambapo ilijumuisha wasanii wakike na wakiume katika kuhamasisha kilimo Africa, Tanzania tuliwakilishwa na Diamond Platnumz pamoja na AY.

Vanessa Mdee ameungana na Victoria Kimani (Kenya), Waje na Yemi Alade (Nigeria), mtoto wa Olver Mtukudz, Selmor Mtukudz pamoja na muigizaji mkubwa kutoka Nigeria, Omotola ambae ni Balozi wa Campaign.

Leo hii Vaanesa na wenzake wametembela kituo cha watoto wa kike wanaoishi katika mazingira yenye utata cha "Miriam Makeba Home for Girls". Wasichana hao huja kuishi katika kituo hicho kwa ajili ya protection.

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging