“Usambazaji ni changamoto kwa wasanii nimeliona hilo baada ya kutengeneza filamu yangu ya Pishu nimeona ni bora nifungue kampuni ya usambazaji ya Kajala Entertainment itaenda kwa wakati na kusambaza kazi zangu,”anasema Kajala.
Msanii huyo anasema kuwa kampuni yake imeajiri wafanyakazi ambao wanatakiwa kufanya kazi na kuingia sokoni sasa endapo kazi moja inachukua muda mrefu kusubiri foleni kwa msambazaji ni tatizo, hivyo anaishauri Serikali kuangalia kazi za wasanii ili waendane na kipato kulingana na umaarufu wao kwani ni vitu viwili tofauti.