Google PlusRSS FeedEmail

MAHARAMIA WAMUINGILIA SNURA

                    Snura Mushi

Mwanamuziki na mcheza filamu Nchini Snura Mushi   amefunguka kwa kusema kuwa mtu aliyeteka namba yake ya simu na kuitumia akiomba fedha na kuitumia kama ni yeye amemfanye apate matatizo na usumbufu usio na manufaa zaidi ya kumkera katika shughuli zake.

“Aliyenifanyia ujinga wa kuharibu namba yangu ya simu na kuanza kuitumia yeye kama mimi si siri amenitia umaskini kwa wakati ule kwani baadhi ya wateja wa kazi zangu walikuwa wakitumia kwa mawasiliano na mimi, lakini nimebadilisha namba nyingine,”anasema Snura.

Msanii huyo anasema aliamua kuibadili namba yake ya simu kwani kila alipojaribu kuirudisha na kuendelea kuitumia mtu huyo aliiteka tena na kuitumia yeye bali anawasisitiza wale jamaa zake waliokuwa na namba ya zamani wasiitumie wala mtu kuwaomba fedha kupitia namba hiyo haitumii wala wasidanganywe na tapeli huyo.

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging