“Aliyenifanyia ujinga wa kuharibu namba yangu ya simu na kuanza kuitumia yeye kama mimi si siri amenitia umaskini kwa wakati ule kwani baadhi ya wateja wa kazi zangu walikuwa wakitumia kwa mawasiliano na mimi, lakini nimebadilisha namba nyingine,”anasema Snura.
Msanii huyo anasema aliamua kuibadili namba yake ya simu kwani kila alipojaribu kuirudisha na kuendelea kuitumia mtu huyo aliiteka tena na kuitumia yeye bali anawasisitiza wale jamaa zake waliokuwa na namba ya zamani wasiitumie wala mtu kuwaomba fedha kupitia namba hiyo haitumii wala wasidanganywe na tapeli huyo.