WIZ KHALIFAH AMTUPIA LAWAMA AMBER ROSE
BAADA ya rapper machine gun Kelly, kutangaza rasmi kwamba anadate na mama Sebastian “Amber Rose” leo Wiz Khalifah ameibuka na kudai kwamba mzazi mwenzie huyo ananjama za kumuharibia “show” yake itakayofanyika Vegas weekend hii.
Wiz amelalamika kile kinachoonekana ni hujuma toka kwa X wake huyo, na kwa mujibu wa post aliyoiweka mapema leo asubuhi kupitia Instagram ni kwamba Amber Rose nae amepanga tarehe na mji mmoja ambapo mtaraka wake atakuwepo pia, kwa ajili ya house party yake atakayoihost.