Google PlusRSS FeedEmail

ALLY KIBA KUPIGA VITA DHIDI YA UJANGIRI


Shirika la Wildaid limemchagua Star wa muziki wa Bongo Flava Ally Kiba, kuwa balozi katika kampeni ya kupambana na Ujangiri nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari katika Hotel ya Sea Clef jana, waziri wa Maliasili na utalii nchini Lazaro Nyarandu amesema kampeni hiyo inalengo la kupambana na Ujangiri nchini, na vijana wa kitanzania wanakuwa sehemu ya ulinzi wa rasilimali za nchi.

“Lengo letu ni kila kijana wa kitanzania anakuwa sehemu ya ulinzi wa Rasilimali za nchi, tumebahatika kuwa na Tembo katika bara la Africa na lazima tupambane na ujangili” alisema Waziri huyo. Ally Kiba ataungana na miss Tanzania wa Zamani, Jackline Ntuyabaliwe Mengi katika ubalozi huo wenye lengo na nia ya kupunguza ujangiri Tanzania. Mtazame Ally Kiba akizungumza hapo chini.

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging