Google PlusRSS FeedEmail

SIR CHRISTOPHER LEE AFARIKI DUNIA

Mwigizaji wa siku nyingi na nyota wa filamu zilizopendwa na wengi Sir Christopher Lee amefariki akiwa na umri wa miaka 93.

Msanii huyo ambaye ni mzaliwa wa Uingereza aliyejenga jina lake kwa kuigiza katika filamu ya Dracula na Frankenstein katika filamu ya kutisha aligiza katika zaidi ya filamu 250.

Alijulikana sana kwa kuigiza kama Scaramanga katika filamu ya James Bond na Evil Wizard Suriman katika filamu ya Lord of the Rings.

Msanii huyo pia ameigiza katika filamu za The Wicker Man na Stars wars.

Inaripotiwa kuwa mwigizaji huyo alifariki siku ya jumapili katika hospitali ya Chelsea Westminster mjini London baada ya kulazwa na ugonjwa wa tatizo la mapafu na moyo.

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging