Google PlusRSS FeedEmail

THE GAME MATATANI

Wiki iliyopita The Game aliachia list ya nyimbo zake zitakazokuwepo kwenye albamu yake mpya ya The Documentary 2 na kuwaweka mkao wakuwa tayari kwa mashabiki wake kununua albamu hiyo iliyosubiriwa kwa hamu kubwa.

Lakini mambo huenda yasiwe kama ilivyopangwa baada ya kuibuka mjadala mpya wa kesi inayomkabili mkongwe huyo wa muziki wa HipHop.

Kwa mujibu wa mwanasheria mmoja The Game anatuhumiwa kutorudisha kiasi cha dola elfu 10 alizochukua kama advance ya show aliyotakiwa aifanye mwezi april kwenye mgahawa na klabu inayojulikana kwa jina la Mass iliyopo Cambrigde pande za USA.

Inaripotiwa baada ya The Game kupokea mkwanja huo alisepa bila ya kupiga show, na alipotafutwa aliendelea kuwazunguusha jamaa.

Mpaka sasa uongozi wa klabu hiyo unafanya mazungumzo na rapa huyo na kubwa zaidi jamaa wanataka mkwanja wao urudishwe la sivyo wanaweza kumuharibia jamaa swala la kurelease albamu yake mpya.

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging