Rapper wa muziki wa kizazi kipya Nchini Young Killer Msodoki,ameamua rasmi kusaka msimamizi wa kazi zake kwa ajili ya kusimamia na kundi lake la matunzo Zero Unit la jijini humo.
Akizungumza Dar es salaam jana Young Killer alisema binafsi anashindwa kufanya vizuri katika fani kutokana na kukosa msimamizi kwani kwa sasa shughuli zake zote za muziki anazifanya yeye mwenyewe
Aidha young Killer alisema kama kuna mtu anaweza kuwa msimamizi wa kazi kuwa msimamizi wa kazi zake na yupo tayari ajitokeze wakae chini pamoja wapange jinsi ya kufanya kazi..