“Filamu ni tofauti na tamthilia, katika filamu kuna changamoto nyingi sana hali ya soko lakini pia maandalizi yake ni gharama, ndio kuna wakati wanaona msanii kama kapotea kumbe anajipanga,”Nora.
Nora anasema kuwa baadhi ya watayarishaji ni waoga kuwashirikisha wasanii wenye uwezo wa kuigiza kwa kuhofia kufunikwa na wasanii hao hivyo wapo tayari kuwapa nafasi ndogo katika kuigiza ili wasifunikwe ili uigize kwa nafasi lazima uwe mtayarishaji.